• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

Zoezi la usajiri wa Anwani za Makazi kupitia mfumo wa kielektroniki wazinduliwa Mkoani Kigoma, Postcode

Posted on: February 9th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Uzinduzi huo umefanyika leo February 09, 2022 Manispaa ya Kigoma/Ujiji ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe.  Thobias Andengenye huku akiwataka wananchi kushiriki zoezi hilo kutokana na faida  zitokanazo na mfumo huo


Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Wananchi wa Mkoa huo kuwasimamia wataalamu na viongozi watakaoshiriki katika  shughuli hiyo kwa kuipa majina mitaa kutokana na Mahitaji ya wakazi wenyeji

Ameendelea kusema kufanyika kwa utambuzì na usajiri wa anwani za makazi kutasaidia kila mtu anayeishi Nchini Tanzania kuwa na anwani halisi ya makazi, utambulisho wa watu wanaoishi katika maeneo husika, usajili wa mali, biashara, na kuboreshwa kwa usajili wa vizazi na vifo

Ameendelea kutaja faida zingine zitokanazo na mfumo huo ikiwa ni pamoja na kufikisha huduma za maendeleo kwa wananchi kulingana na mahitaji yao, kupatikana kwa huduma za manunuzi kidigitali, Huduma za dharura, kama vile polisi, zimamoto na magari ya wagonjwa, zinaweza kutambua maeneo yenye dharura na kuyafikia kwa haraka, na kurahisisha  zoezi la Sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika Mwezi August mwaka huu

Mkuu huyo wa Mkoa amehitimisha kwa kuwaagiza Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Wakuu wa Idara na vitengo kusimamia zoezi hilo kikamilifu kutokana na faida zitokanazo na mfumo huo

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Ndugu. Rashid Mchatta awali akimkaribisha Mkuu huyo wa Mkoa amesema yupo tayari kusimamia zoezi hilo kwa Wilaya zote za Mkoa huo  kwa kushirikana na  Wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa  huku akisema zoezi hilo litakamilika mapema mwezi May, 2022 kama ilivyoagizo kutokana na Miji, Vijiji na Vitongoji vya Mkoa huo vingi kuwa katika mipangilio iliyobora tangu awali

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Esther Alexander Mahawe amesema usajiri wa Anwani za Makazi utaleta Mapinduzi makubwa ya maendeleo katika Wilaya na makazi ya wananchi kwa kuhakikisha huduma  za Elimu, Afya na uwekezaji wa Miundombinu ya kimaendeleo inafanyika pasipo kuwa na upendeleo wowote bali kulingana na Mahitaji ya Jamii

Utambuzì wa Anwani za makazi unafanyika kwa kubandika namba za makazi, jina la barabara au Mtaa na namba ya postikodi itakayosaidia kufahamu eneo husika kidigitali, maeneo ya biashara, vitu , watu, Na  Ofisi zote kusajiliwa katika mfumo huo wa kidigitali

 Uzinduzi huo umehudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa, viongozi wa vyama vya Siasa, Wakuu wote wa Wilaya , Meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri na Taasisi za Serikali na zisizo za Serikali, Waheshimiwa Madiwani, Watendaji kata na Mitaa, Wenyeviti wa Mitaa, Waandishi wa habari, wasanii, na  Wananchi


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa